Hata kabla ya matokeo rasmi ya uchaguzi nchini Kenya ujumbe wa kumpongeza mshindi wa urais umechapishwa katika akaunti ya Twitter ya Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza.
Bw Nkurunziza anaonekana kumpongeza Rais Kenyatta.
Lakini labda ni afisa wa mawasiliano wa Nkurunziza ambaye ameandika ujumbe huo.
Kwenye maelezo katika ukurasa huo wa Twitter, ambao una wafuasi 59,000, ujumbe wa moja kwa moja kutoka kwa rais huyo unafaa kuwa na sahihi ya PN.
On behalf of all Burundians, I congratulate President elect @UKenyatta and the people of Kenya. Looking forward to strengthen our relations.— Pierre Nkurunziza (@pnkurunziza) August 10, 2017
