Mgombea Urais wa pili Kenya akubali kushindwa

Mgombea wa pili wa urais nchini Kenya Dkt Ekuru Aukot amekubali kushindwa.

Ndiye wa pili kutangaza kushindwa baada ya Dkt Japheth Kavinga Kaluyu kukubali kushindwa jana.

Dkt Aukot amesema anaamini "Wachache walipata fursa ya kusikika, na wengi walishinda."

"Jiwe la Daudi halikumuweza Goliathi wakati huu, na asiyekubali kushindwa si mshindani," amesema.

Ametoa wito kwa Raila: "Hatungekuwa hapa bila wewe, demokrasia ya Kenya ya sasa haiwezi kuzungumziwa bila wewe kuwepo.

Kenya yataka kusonga mbele, Wakenya wanataka kurejelea shughuli za kawaida.

Kwa kuchunguza Fomu 34A tulizopata, tumegundua kwamba hakuna sababu ya kuamini kuna chochote kitabadili matokeo ya sasa."

Amemtaka Rais Kenyatta, akitangazwa mshindi, aunde serikali yake kwa kujumuisha wote.

Dkt Aukot amedokeza kwamba huenda akawania tena urais mwaka 2022.
Mpya zaidi Nzee zaidi