DR Congo:Wapinzani 12 waliotuhumiwa kumkashifu Rais Kabila waachwa huru

Wapinzani 12 waliotuhumiwa kumkashifu rais Kabila waachwa huru Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Wapinzani hao 12  walikamatwa katika maandamano dhidi ya rais Kabila yaliofanyika Desemba 19 mwaka 2016.

Waandamanaji hao waliandamana wakimtaka rais Kabila  kuondoka madarakani.

Mahakama ya Kivu-Kaskazini Mashariki mwa  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imewaacha huru  wapinzani hao.

Maandamano hayo yalifanyika wakati ambapo muhula wa rais Kabila  ulikuwa umefikia ukingoni.

Miongoni mwa wapinzani waliokamatwa na kuachwa huru alikuemo mwanamke mmoja.
Mpya zaidi Nzee zaidi