https://monetag.com/?ref_id=TTIb Mbunge wa Songea mjini afariki dunia | Muungwana BLOG

Mbunge wa Songea mjini afariki dunia

Mbunge wa Songea Mjini kupitia CCM, Leonidas Gama amefariki dunia katika hospitali ya Peramiho mkoani Ruvuma akipatiwa matibabu.

Taaifa za kifo cha mbunge huyo zimethibitishwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Ruvuma, Oddo Mwisho, na kusema kwamba marehemu alifariki dunia usiku wa saa 6 kuamkia leo.

Oddo Mwisho ameendelEa kwa kusema kwamba alipata taarifa kwamba Leonidas Gama alianguka ghafla usiku wa jana kutokana na tatizo la presha na kukimbizwa hospitali ya Peramiho, mpaka pale umauti ulipomkuta.

LeonidaS Gama amewahi kuhudumu kama mkuu wa WIlaya sehemu mbali mbali hapa nchini, na mwaka 2015 kugombea ubunge wa jimbo la Songea Mjini kupitia CCM.