DC Wa Nyerere Apigwa

Aliyewahi kuwa Mkuu Wa Wilaya katika Mikoa mbalimbali nchini Juma waziri amuangukia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, kwa kumtaka aingilie kati kufuatia nyumba yao kutapeliwa na mtu mmoja aitwaye Mpango waliyedai kuwa naye alimuuzia  raia wa China ambaye alikuwa mpangaji wa nyumba yake.


Akizungumza na waandishi wa habari leo, mtoto wa mzee huyo aitwaye Maida Waziri amesema kuwa nyumba  yao imetapeliwa na mpangaji wao aliyekuwa amepangishwa kwa kipindi cha zaidi ya miaka kumi na baada ya mkataba wa malipo ulipoisha alitakiwa kulipia pango lingine lakini alikaidi akidai kuwa nyumba ni ya kwake  na kwamba aliuziwa.

Amesema kuwa kabla ya mpangaji huyo kuuziwa nyumba na watu wasiojulikana, familia hiyo ilipata taarifa kwamba nyumba ilitaka kuuzwa na fedha zingepita benki ya Twiga Bancorp,  hatua iliyowalazimu kupeleka zuio lakini benki hiyo haikufuata maelekezo hayo.

Maida amefafanua kwamba baba yake amekuwa mtumishi wa umma kwa takribani zaidi ya miaka 30 na alijenga nyumba zake wakati  akiwa mtumishi wa serikali enzi hizo, pia nyumba hiyo hiyo anayodai kudhurumiwa amejenga kwa kipindi cha miaka 30 ambapo kwa sasa ana umri wa miaka zaidi ya 90.
Mpya zaidi Nzee zaidi