https://monetag.com/?ref_id=TTIb Ongeza Mavuno Kwa Matumizi Sahihi Ya Mbolea | Muungwana BLOG

Ongeza Mavuno Kwa Matumizi Sahihi Ya Mbolea

Somo la Mbolea
Yara Tanzania Ltd ni kampuni inayojiusisha na utengenezaji, usambazaji, uuzaji na utoa elimu kuhusu Mbolea za mazao mbalimbali.

Mbolea katika maana nyepesi ni Lishe ya mmea. Hivyo ua na vii ni lishe ambavyo ni muhimu ktk ukuaji, uotaji, uzalishaji na ulinzi wa ubora mmea.

Mbolea zipo katika makundi mawili

  1. Mbolea za asiri (organic) mf. Samadi, Mboji n.k
  2. Mbolea za viwandani (Inorganic)
  3. DAP, Winner, Tsp, SA, n.k


Mbolea za viwandan pia naweza kuzigawa katika makundi haya

  1. Mbolea za moja kwa moja. Mf UREA, DAP.
  2. Mbolea za mchanganyo. Mf NPK utoa viin lishe zaidi ya viwil, NPK utoa viini lishe 3 vikuu katk ukuaji wa mmea hvyo ni BORA kuliko DAP, CAN na SA na kzl (utoa viini lishe viwil ama kmoja) kwa maana hiz zinaitaji ujue kiini lishe kipi kimekosekana kwenye udogo.

Naweza pia nikagawanya makundi ya mbolea kama ifuatavyo. Hapa NISIELEWEKE. VIBAYA musome munielewe sina maana kua mbolea zingine zisitumike hapana, zitatumika kulingana na hitaji la udongo wako baada yakufanya soil analysis (tafiti za ubora wa udongo-kwa lugha ya mkulima) naomba kuendelea na makundi hayo.

1. Mbolea nzuri.
Mbolea nzuri huwa na sifa zifuatazo.

  • Uyeyuka kwa uraisi
  • Zinakua na lishe linganifu kwa mmea
  • Hazina madhara katika udongo (nyongo na tindikali /Soil pH)
  • Zinakua na viini lishe zaidi ya vitatu kwenye lishe linganifu.


2. Mbolea mbaya.
Mbolea mbaya bila shaka ni kinyume cha mbolea nzuri.
Kwa misingi hiyo sasa mbolea za asiri zinakua katika kundi la pili (mbaya-nisieleweke vibaya naz pia zna uzuri wake itategemea lengo) kwakua hazina lishe linganifu na pia zinachelewa kuyayuka maranyingine.

Mbolea kama DAP, CAN, SA, Tsp, n.k (NPK-angalau hii) hizi nazo zinakua kwenye kundi hili (mbaya).

Sababu-Viini lishe vichache (viwil kimoja ana vitatu ) yaani pana N, K, P, Ca, S tena hapo kwny CAN hakuna Ca ndio maana hawaandiki kwenye mifuko Ca iliyopo kwenye CAN ni insoluble (Hisiyoyeyuka hivyo mmea haupat Ca)

SA ina salfa (S) nyingi kulikoinayoitajika na mmea hivyo uchachua udongo nakusababisha udongo kutoweza kutoa P kwaajiri ya mmea (P fixation).

SA kama sijakosei zimeandika 27% S wakati mimea mingi inahitaji almost 5.6% ya Salfa hvyo % znazobaki zinachachua udongo na pia mimea inahitaj 40→46% ya N mbolea za asiri mara nyingine uwa na zaidi ya hii ama pungufu (utoa unbalanced nutrition).

Yara Tz Ltd Kama kampuni Mama ina mbolea za CAN, DAP, UREA, na SA kama makampuni mengine, hizi ni mbolea ambazo makampuni mengi utengeneza TZ.

Kwakua ni YARA ni kampuni inayofanya tafiti zakutosha dunian kote imekuja na mbolea mpya ambazo utoa na kuupa mmea viini lishe linganifu (ile inayostahili na kuitajika na mmea kwa kipindi mmea upo shambani hadi kuvunwa)

Mbolea hizi ni kama zifuatazo japo kwa uchache kwa maana wana mbolea nyingi kote duniani.
Niweke katika makundi haya sasa kwa ufahamu nilio nao kwenye mbolea.

MBOREA NZURI
  • YARA MILA - Kundi hili ni NPK iliyo boreshwa (yenye lishe linganifu, kuyeyuka vizuri na kutokua na madhara kwenye udongo kama utafuata maelekezo sahihi) na inaviini lishe vingine, hizi mbolea utumika kwa kupandia hata kukuzia mazao.
  • Mf. YARAMILA WINNER - Kwa ajiri ya mbogamboga. NPK yenye virutubisho vitano vya ziada ,Z, Bo, Mn, S na Mg.
  • YARAMILA CEREAL - Kwa ajiri ya Nafaka zote.
  • YARABELA - Hizi ni CAN zilzoboreshwa na kua na lishe linganifu na pia utumika kama mbolea ya kukuzia.
  • Mf. YARABELA SULFAN - Kukuzia nyanya hata nafaka. ni CAN yeye Ca inayoyayuka na N, S.
  • YAYA VITA- Hizi ni mbolea zenye trace elements (viini lishe vidogo sio vikuu kama Bo, Mg, Zn, Mo, n.k Vipo 11 na pia ina viini lishe vkuu NPK). Mbolea hizi utumika kwenye majani kuusaidia mmea kupata lishe nje ya udongo.
  • Mf YARAVITA TRACEL BZ - Mbogamboga na nafaka pia.
  • YARA VERA - Hizi ni mbolea za Urea zilizoboreshwa zina Salfa na N.
  • Mf. YARAVERA AMIDAS na YaraVera Amigran. hiz utumika kukuzia nafaka.
  • YARALIVA - Hizi ni Quality improved fertilizer (mbolea kwa ajiri ya kuboresha ubora na maisha lufani ya zao lako) zina Ca kwa wingi inayoyeyuka, N na Boron kqa ajiri yakunenepesha, kuunda gamba gumbu lakuung'aa na kuweza usafirshaji na kizui kurojeka/kubunguriwa kirahisi kwa mazao.


Mf YaraLiva Nitrabor
Kutokaa na somo hilo utajifunza kua mbolea inaweza ikawa na viin lishe vichache katka lishe linganifu HIVYO ikawa ni bora zaidi ya ile yeny viini lishe/virutubisho vingi visivyolinganifu.
Pia unaweza ukawa na mbolea yeye virutubisho  sahihi lakini ikawa haiyeyuki kirahisi.

Ni muhimu mkulima akafahamu aina na udongo wake, aina na viini lishe vilivyopo na vinavyokosekana na hivyo itasaidia kujua aina ya mbolea inayoitajika kiasi cha mbolea na aina ya zao utakaloitajika kupanda.

Mmea uliopata lishe bora ni lazima ulindww inavyotakiwa dhidi ya wadudu na magonjwa( matumizi ya madawa) na wanyama waalibifu.