Ibrahimovic afurahia maisha LA Galaxy

Mshambuliaji mkongwe wa Sweden, mwenye umri wa miaka 36, Zlatan Ibrahimovic akifurahia kwenye mazoezi ya LA Galaxy jana baada ya kujiunga nayo rasmi kutoka Manchester United ya England kwa kusaini mkataba wa miezi 18. Ibra anaweza kuanza kucheza Ligi ya Marekani, MLS leo dhidi ya mahasimu wa Los Angeles, LAFC.