Shambulizi la bomu mbele ya jengo la bunge na wizara ya mambo ya ndani

Mlipuko wa bomu umetokea  karibu na jingo la bunge na wizara ya mambo ya ndani mjini Mogadishu nchini Somalia. Shambulizi hilo limetokea katika kituo cha kulinda usalama ambapo gari lililokuwa na vilipuzi kulipuka Jumapili majira ya jioni. Nur Mohamed , Kiongozi wa jeshi la Polisi mjini Mogadishu ametoa taarifa kuwa mlipuko huo umetokea katika kituo cha usalama cha Sayidka.

Abdikadir Abdirahman , Mkurugenzi wa shirika la Amin la kutoa huduma ya kwanza amesema kuwa mtu mmoja amefariki na mwingine mmoja amejeruhiwa.
Mpya zaidi Nzee zaidi