Msichana anatafutwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuchoma moto nyumba


Na. Thabit Madai,Zanzibar.

Msichana aliejulikana kwa jina moja Asma mkazi wa Mwera anatafutwa na Jeshi la polisi Mkoa wa mjini magharib kwa tuhuma za kuchoma moto nyumba ya Mama aliejulikana kwa jina la Zubeda Yahya abdallah hadi sasa chanzo cha kuchoma moto nyumba hiyo bado hakijajulikana.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa mjini magharb Unguja Thobias Gesauda Sedoyeka alisema jeshi la polisi mkoa wa mjini  linaendelea kumtafuta mtuhumiwa huyo aliekimbia kwa tuhuma za kuchoma moto nyumba ya bi zubeda yahya abdallah miaka 22  mshirazi wa mwera.

Alisema moto huo umesababisha hasara ya kuunguza vitu vingi vilivyomo ndani  ya nyumba hiyo ambapo hasara yote iliyotokea inakisiwa jumla shilingi million mbili na laki tano za kitanzania.

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Kilimo cha Bamia