Mambo ya kuyaepuka katika ufugaji wa kuku


Ndugu mfugaji ni ukweli usiopingika wala kujadilika kuwa katika ufugaji kuna baadhi ya mambo wafugaji tunayafanya lakini hayakupaswa kufanyika, yafuatayo ni ya kujiepusha nayo katika ufugaji:-


  • Kuacha banda chafu
  • Kuleta kuingiza kuku wageni bila kujua historia ya chanjo walipotoka.
  • Kuuza kuku wagonjwa.
  • Kuchinja kuku wagonjwa.
  • Kununua kuku wagonjwa.
  • Kutupa kuku waliokufa porini.
  • Kununua chanjo kwa wauzaji wanaofahamika kuwa hawana solar power au jenereta.
  • Kutibu kwa mazoea bila kuwasiliana na Afisa Mifugo.
  • Kutembelea mabanda ya jirani bila kuchukua tahadhari.