Ndugu mfugaji ni ukweli usiopingika wala kujadilika kuwa katika ufugaji kuna baadhi ya mambo wafugaji tunayafanya lakini hayakupaswa kufanyika, yafuatayo ni ya kujiepusha nayo katika ufugaji:-
- Kuacha banda chafu
- Kuleta kuingiza kuku wageni bila kujua historia ya chanjo walipotoka.
- Kuuza kuku wagonjwa.
- Kuchinja kuku wagonjwa.
- Kununua kuku wagonjwa.
- Kutupa kuku waliokufa porini.
- Kununua chanjo kwa wauzaji wanaofahamika kuwa hawana solar power au jenereta.
- Kutibu kwa mazoea bila kuwasiliana na Afisa Mifugo.
- Kutembelea mabanda ya jirani bila kuchukua tahadhari.