Wachezaji wa Yanga wazuiwa kuzungumza

Kocha Msaidizi wa Yanga, Noel Mwandila amewazuia wachezaji wake kuzungumza chochote na waandishi wa habari.

Mwandila amewazuia wachezaji wake na badala yake amewataka waelekeze nguvu zao zote mazoezini kuelekea msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

Yanga inaendelea na mazoezi kujiandaa na tamasha la Wiki ya Mwananchi litakalofanyika Uwanja wa Taifa August 4 2019.

Tamasha hilo litafanyika ambapo timu hiyo itacheza mchezo wa kirafiki na AS Vita