Balozi wa Uturuki Nchini afanya mazungumzo na Waziri wa Elimu


Balozi wa Uturuki Nchini Tanzania Ali Davutaglu ( mwenye tai nyekundu) amemtembelea na kufanya mazungumzo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako ofisini kwake Dodoma leo.

Mazungunzo yao yalilenga katika kuimarisha ushirikiano katika sekta ya elimu ikiwemo uwekezaji katika ujenzi wa Shule na vyuo nchini.

Balozi Davutaglu ameambatana na mwekezaji katika sekta ya Elimu, Oguz Hamza Yilmaz kutoka Maarif Foundation Uturuki (mwenye tai ya bluu).