Rais wa Uturuki Recep Tayyıp Erdoğan azungumza kwa njia ya simu na rais wa Marekani Donald Trump.
Katika mazungumzo yoa viongozi hao wawili wamejadili kuhusu ushirikiano katikasekta ya biashara na kiwango cha dola bilioni 100.
Vile vile katika mazungumzo yao viongozi hao wawili wamezungumza kuhusu ushirikiano kati ya mataifa yao hayo mawili katika nyanja tofauti.
Kuhusu hali inayoendelea nchini Libya, viongozi wa mataifa hayo mawili wameafikiana kuendelea na ushirikiano katika kutafuta suluhu kunako mzozo wa Libya.