Zaidi ya wakimbizi 72 000 kutoka nchini Burundi walipewa hifadhi nchini Rwanda kufuatia ghasia ambazo zilizuka nchini humo mwaka 2015.
Kundi la wanajeshi waliotaka kupindua serikali ya rais Pierre Nkurunziza walisababisha machafuko nchini humo baada ya maandamano yaliokuwa yakÅŸfanyika nchini humo.
Watu wengi walilazimika kuyahama makazi yao huku wengine kukimbilia katika mataifa jirani ukanda wa Afrika Mashariki ikiwemo nchini Rwanda.
Zaidi ya watu 72 000 walikimbilia nchini Rwanda mwaka 2015.
Ni zaidi ya wakimbizi 500 kutoka nchini Burundi wamechukuwa uamuzi wa kurejea nchini Burundi.
Wakimbizi hao walÅŸorejea nchini Burundi walikuwa wakiishi katika kambi ya wakimbizi ya Mahama.
Kulingana na taarifa iliotolewa na wizara ya mambo ya ndani ya Burundi inayoongozwa na Gervais Ndirakobuca, wakimbizi ha wamerejea nchini Burundi Alkhamis.
