Zaidi wa wakimbizi 500 warejea Burundi kutoka nchini Rwanda




Zaidi ya wakimbizi   72 000 kutoka nchini  Burundi walipewa hifadhi nchini Rwanda  kufuatia ghasia ambazo zilizuka nchini humo mwaka  2015.

Kundi la wanajeshi waliotaka kupindua serikali ya rais Pierre Nkurunziza walisababisha machafuko nchini humo baada ya maandamano yaliokuwa yakÅŸfanyika nchini humo.

Watu wengi walilazimika kuyahama  makazi yao  huku wengine kukimbilia katika mataifa jirani  ukanda wa Afrika Mashariki ikiwemo nchini Rwanda.

Zaidi  ya watu 72 000 walikimbilia nchini Rwanda mwaka  2015.

Ni zaidi ya  wakimbizi 500 kutoka nchini Burundi wamechukuwa uamuzi wa kurejea nchini Burundi.

Wakimbizi hao walÅŸorejea nchini Burundi walikuwa wakiishi katika kambi ya wakimbizi ya Mahama.

Kulingana na taarifa iliotolewa na wizara ya  mambo ya ndani ya Burundi  inayoongozwa na Gervais Ndirakobuca, wakimbizi ha wamerejea nchini Burundi Alkhamis.

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi