Alikiba naye apita njia za Harmonize, Daimond


Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), John Pombe Magufuli amefunga midomo ya watu baada ya kumvalisha kofia msanii Aalikiba.

Rais Magufuli alifanya tukio hilo leo Jumatano Septemba 16 katika mkutano wa kampeni za urais wa chama hicho mjini Bukoba.

Alikiba amevalishwa kofia na Rais Magufuli leo Jumatano ikiwa ni siku chache tangu afanye hivyo kwa msanii Harmonize na Diamond ambaye yeye alivishwa kofia alipotumbuiza kwenye kampeni za CCM Uwanja wa Kirumba mkoani Mwanza.

Hata hivyo, ni kama mgombea huyo ameyasikia majigambo ya pande hizo mbili, na leo Septemba 16, 2020 ameamua kusawazisha kwa kumvalisha kofia @officialalikiba.

Kama alivyofanya kwa #Diamond na #Harmonize, Rais Magufuli alisimama na kumuita #Alikiba kisha kumvalisha kofia na kumuacha ashuke chini kuendelea kutumbuiza.

Post a Comment

0 Comments