Bobi Wine asema 'Museveni anakabiliwa na kizazi chenye hasira na njaa'



Mgombea urais wa upinzani nchini Uganda Robert Kyagulanyi, maarufu Bobi Wine, amesema Rais wa Yoweri Museveni anakabiliana na kizazi ambacho kitafanya kila iwezelo kupigania uhuru.


Alisema hayo katika hafla ya maombi iliyoandaliwa katika makao makuu ya chama chake kuwaomea watu waliouawa katika maandamano ya siku mbili yaliyokumba nchi, siku moja baada ya kuachiwa kutoka kizuizini.


Akimlenga moja kwa moja kiongozi wa nchi moja kwa moja Bobi Wine alisema Bwana Museveni anakabiliwa na kizazi ambacho kina njaa na hasira kwa wakati mmoja.


Hakuna kiwango chochote cha mabomu ya machozi au mateso ambacho kitawaogopesha, aliongeza.


Mgombea huyo wa urais amesema mashambulio yaliyofanywa dhidi ya raia wiki hii yameweka wazi udhalimu wa serikali ya sasa iliyo madarani.


Akiwahutubia wafuasi na maafisa wa chama, alisisitaiza kwamba damu ya raia wasiokuwa na hatia iliyomwagika wiki hii haitaenda bure, na kuongeza kuwa haki itatekelezwa.


Jumamosi asubuhi, magari ya vikosi vya usalama yaliegeshwa katika maeneo tofauti mjini Kampala huku askari wakishika doria katika maeneo karibu na makao makuu ya chama cha upinzani cha People's Power.


Polisi imetangaza kuwa ni watu 28 waliofarika katika maandamano ya siku ya Jumatano na Alhamisi, japo vyombo vya habari nchini vinanukuu vyanzo vya hospitali kuu kwamba idadi ya waliofariki ni watu 37.


Bobi Wine aliachiwa kwa dhamana siku ya Ijumaa, baada ya kushtakiwa kwa kukiuka kanuni za kudhibiti kusabaa kwa virusi vya corona. Anakabili wa kifungo cha hadi miaka saba gerezani akipatikana na makosa.


Lakini kwa sasa, mwanamuziki huyo na mwanasiasa amesema yuko tayari kurejelea kampeni zake kuanzia Magharibi mwa Uganda.


Mnamo mwezi Juni Bobi Wine aliapa kukiuka marufuku ya mikutano ya kampeni wakati wa janga la corona. Alimshtumu Rais Museveni kwa "kuogopa watu".


Msmaji wa serikali ya Uganda Don Wanyama ameambia BBC kuwa maafisa "hawengeweza kutualia na kuangalia ghasia kufanyika j".


Pia amesema RaiS Museveni "ametii marufuku iliyowekwa na Tume ya Uchaguzi na Wizara ya Afya".


Human Rights Watch linasema ni wazi kwamba mamlaka za Ugandan zinatumia mwongozo wakuzuia Covid-19 kukandamiza upinzani na kuongeza kuwa chama tawala kimefanya kampeni kubwa.


Post a Comment

0 Comments