Manara awavaa Yanga "Malalamiko ya nini wakati hyo saa moja tutacheza wote?"

 Wakati Yanga wakiwa tayari wameshawasili uwanjani na wakijipanga kuanza kupasha misuli. Msemaji wa Simba Haji Manara ametoa kauli kwamba wao wapo tayari kucheza na Yanga muda wowote.

Kupitia ukurasa wake wa instagramu Manara ameandika;

Malalamiko ya nn wakati hyo saa moja tutacheza wote? Hata cc hatukufurahia mabadiliko hayo ya ghafla , lakini hatuna budi kukubaliana na uamuzi wa Mamlaka !!

Simba ipo tayari kucheza hata usiku wa manane, as longer us TFF na Wizara wamesema, We are Ready,,,,Raha ya kiporo ukile usiku kabla kukuchwa 🤪🤪

Au kama vp suseni tu kama ilivyo ada yenu wazee wa kulalamika hovyo hovyo 😀😀




Post a Comment

0 Comments