F JWTZ lakanusha taarifa zinazosambazwa kuwa jeshi hilo linajihusisha na maandamano | Muungwana BLOG

JWTZ lakanusha taarifa zinazosambazwa kuwa jeshi hilo linajihusisha na maandamano



 


Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania JWTZ limekanusha taarifa zinazosambazwa katika mitandao ya kijamii yenye maudhui ya maandamano yenye lengo la kuwahadaa wananchi na kusababisha vurugu na kubainisha kuwa taarifa hizo si za kweli na hazijatolewa na JWTZ huku likitoa onyo kali kwa wanaojihusisha na vitendo hivyo.

Katika taarifa kwa umma iliyotolewa na Jeshi hilo imesema Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania JWTZ linauarifu umma wa watanzania kuwa kuna tangazo linaloonekana likisambaa mitandaoni lenye maudhui ya maandanamo kuwa ni uzushi wenye lengo la kuwahadaa wananchi na kusababisha vurugu na uvunjifu wa amani nchini hivyo taarifa hizo zipuuzwe.

Taarifa hiyo imekemea tabia inayokithiri ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii inayolihusisha jeshi na siasa kwa lengo la kupotosha umma na kuzua taharuki.

Taarifa hiyo imeendelea kusema kuwa JWTZ litaendelea kushirikiana na vyombo vingine vya usalama na mamlaka ya mawasiliano Tanzania kuwabaini na kuwachukuria hatua za kisheria wote wanaojihusisha na upotoshaji huo.

Chapisha Maoni

0 Maoni