Serikali ya China
imetangaza uungaji mkono wake kwa serikali ya Nigeria katika juhudi zake za
kurejesha usalama na amani nchini humo. Hayo yamesemwa na Wang Runxu, afisa wa
ngazi za juu wa jeshi nchini China
akiwa Nigeria na kusisitiza
kuwa, China ni muungaji
mkono mkubwa kwa juhudi za serikali ya Abuja
katika kupambana na ugaidi. Afisa huyo wa kijeshi ameongeza kuwa, ushirikiano
wa nchi yake na Nigeria
katika wigo wa usalama, unazidi kuimarika.
Askari wa China
wako nchini Nigeria
kupitia mpango wa kutoa mafunzo kwa jeshi la nchi hiyo. Mashambulizi ya kundi
la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram, ni changamoto kuu ya usalama nchini Nigeria .
Kundi hilo lilianzisha
mashambulizi yake ya kigaidi tangu mwaka 2009, na hadi sasa maelfu ya watu
wameuawa na zaidi ya milioni moja kuwa wakimbizi ndani na nje ya mipaka ya
taifa hilo la
magharibi mwa Afrika. Mwaka huu wa 2015, kundi hilo
lilipanua zaidi wigo wa mashambulizi yake hadi katika nchi za Niger , Chad
na Cameroon , suala ambalo
lilitoa changamoto kwa serikali ya nchi hizo kuunda muungano wa kijeshi dhidi
ya kundi hilo .
