Haji Manara
Mkuu wa Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo Haji Manara amesema klabu hiyo imeamua kukubali ombi la baraza hilo, ili kuweka mambo sawa kuelekea mkutano huo na kutoa ufafanuzi kwa jambo lolote ambalo litakuwa halijaeleweka kuelekea katika mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji wa timu hiyo.
Manara amesema kuwa kikao hichokimepangwa kufanyika wakati wowote kati ya leo au kesho, na kwamba uongozi una imani kubwa kwamba wataelewana, huku akisisitiza kuwa mkutano mkuu wa klabu hiyo uko palepale, na tayari maandalizi yamekamilika.
Katibu wa Baraza la Bodi la Wadhamini wa Simba, Hamisi Kilomoni (katikati) akizungumza na wanahabari wiki iliyopita
