Kiongozi wa waandalizi wa uchaguzi wa Umoja wa Afrika (AU) Thabo Mbeki amesema hawawezi kuzungumzia madai ya upinzani kwamba mitambo ya IEBC ilidukuliwa.
Kiongozi huyo mstaafu wa Afrika Kusini amesema jukumu la waangalzii ni kuangalia shughuli ya uchaguzi inavyofanyika.
"Sisi si wachunguzi wa uchaguzi," amesema.
Iwapo tungeona kitu kikifanywa vibaya, kinyume na sheria za Kenya na viwango vya AU, tungeingilia kati.
Katika baadhi ya visa, NASA wamewasilisha malalamiko kwetu kuhusu uchaguzi, mfano kupatikana kwa sajili ya wapiga kura na usalama pia - mfano kusafirishwa kwa maafisa takriban 40 wa polisi kwenda kwingine.
Tuliangazia haya, na baadhi tukawapasha IEBC kuhusu malalamisho ya sajili na kuhusu polisi tukawasiliana na kukutana na waziri wa usalama Dkt Fred Matiang'i.
