Nigeria: Shambulizi laua watu19

Watu takriban 19 wameuawa katika  shambulizi linalodhaniwa kuwa la kulipiza kisasi katika moja ya vijiji nchini Nigeria.

Kwa mujibu wa habari,shambulizi  hilo limetokea siku tatu baada ya kijana kutoka katika kabila ya Fulani aliyekuwa amepotea kukutwa amekufa katika kijiji cha Ancha

Mkuu wa polisi  amesema kuwa uchunguzi zaidi unaendelea lakini mpaka sasa inaonekana dhahiri kuwa shambulizi limefanywa na wachungaji wanyama wa kabila la Fulani ,kulipiza kisasi cha kijana wa Fulani aliyekutwa kakatwa kichwa  baada ya kupotea mnamo Agosti 3.

Ripoti zinaonyesha kuwa kati ya waliopoteza maisha ni watu wazima 13 huku  wengine 6 wakiwa ni watoto.

Watu wengine watano wameripotiwa kujeruhiwa katika shambulizi hilo.
Mpya zaidi Nzee zaidi