Mama Kanumba kumtembelea Lulu Mahakamani

 Frola Mtegoa.

MAMA wa staa wa filamu Bongo, marehemu Steven Kanumba, Frola Mtegoa amesema kuwa, kutokana na matatizo yaliyompata staa wa filamu Bongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ baada ya kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili, amekuwa akimuonea huruma na anajipanga kumtembelea gerezani.

Akipiga stori na Ijumaa, Mtegoa alisema watu wengi wamekuwa wakihisi kuwa ana chuki na Lulu, lakini moyo wake unampenda na kama isingekuwa sheria kuhitaji Lulu kufungwa basi yeye asingekuwa na tatizo naye.
Staa wa filamu Bongo Elizabeth Michael ‘Lulu’

“Sina chuki na Lulu, tulikuwa karibu lakini nafikiri watu wake wanaozunguka ndiyo waliosababisha ukaribu wetu kuparanganyika. “Lakini moyoni ninampenda na kiimani mimi ni Mkristo.

Kwa hiyo siwezi kufurahi kuona mwenzangu anapata matatizo, ipo siku nitamtembelea gerezani!” alisema mama huyo.