Rais Magufuli ateuliwa, mwenyewe aukubali uteuzi huo


Rais John Magufuli, amepokea rasmi taarifa ya uteuzi wa kuwa makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC),  kwa mwaka mmoja kuanzia Agosti 2018 - Agosti 2019.

Taarifa hiyo imekabidhiwa kwa Rais Magufuli leo Oktoba 8, 2018 na Katibu mtendaji wa Jumuiya hiyo Dkt. Stergomena Tax, ambaye amesema amekutana na Rais Magufuli ili kumpa taarifa ya uteuzi uliofanyika kupitia mkutano mkuu wa 38 wa SADC ambao ulifanya Agosti 17-18, 2018 mjini Windhoek nchini Namibia.


Mpya zaidi Nzee zaidi