Fainali ya Miss Tanzania 2019, kufanyika tarehe...


Fainali za Mashindano ya urembo ya Miss Tanzania 2019 chini ya uongozi mpya wa Kampuni ya The Look ambayo yalianza mapema mwezi April 2019 yatafikia kilele chake tarehe 23 Agosti 2019 katika Ukumbi wa New Millennium Towers LAPF uliopo eneo la Makumbusho jijini D’salaam.

Washiriki wapatao 20 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania tayari wapo kambini tangu tarehe 12 Agosti 2019 wakijiandaa na kinyang’anyiro hicho cha kuwania taji hilo.

Kufanyika kwa Fainali hizi ni hitimisho ya mashindano ya mikoa .na kanda ambayo yalifanyika katika kipindi cha kuanzia mwezi April hadi Julai 2019.

Wakiwa kambini Warembo hawa wameshiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii, ikiwa ni pamoja na kutembelea katika Kituo cha Watoto wetu Tanzania kilichopo eneo la Mbezi Mwisho jijini D’salaam Kituo ambacho kinatunza watoto wanaoishi katika Mazingira magumu.

Wakiwa katika Kituo hicho warembo wetu wameweza kuwafariji watoto hao kwa kucheza nao Michezo ya aina mbalimbali na kula nao pamoja.

Warembo pia wameshiriki katika mashindano madogo yajulikanayo kama Fast Tract na kuweza kufanya vizuri katika mashindano hayo ya kumtafuta

Mrembo mwenye kipaji – Miss Talent
Mrembo mwenye mvuto katika picha – Miss Photogenic
Mrembo mwanamitindo – Top Model
Mrembo mwanamichezo – Top sports woman
Mrembo chaguo la watu – Miss Personalit
Warembo hao wapo ambao wameingia katika hatua ya Tano Bora na washindi katika mashindano hayo watatangazwa katika Fainali usiku wa tarehe 23 Agosti 2019.