Mbwana Samatta apatwa na majeraha ya goti


Nahodha wa Taifa Stars, Mshambuliaji Mbwana Samatta, Jumapili alipata majeraha ya goti kwenye mechi dhidi ya Burundi na kumlazimu kocha kufanya mabadiliko dakika ya 106 akiingia Himid Mao.

Mara baada ya kumalizika kwa mchezo alikwea pipa (Jumatatu) na kurejea Ubelgiji katika klabu yake ya Genk.

Baada ya kufika Ubelgiji, Kupitia ukurasa wake rasmi wa mtandao wa Instagram Samatta ameeleza kuwa tayari amefanyiwa vipimo vya MRI katika goti.