https://monetag.com/?ref_id=TTIb Mbunge wa Babati Mjini aandaa Semina ya Ujasiriamali Kwa Wananchi wake | Muungwana BLOG

Mbunge wa Babati Mjini aandaa Semina ya Ujasiriamali Kwa Wananchi wake


Na John Walter, Babati.

Mbunge wa Jimbo la Babati Mjini (CCM) Mheshimiwa Paulina Gekul ametoa wito  kwa wakazi wa mji wa Babati  kutumia fursa mbalimbali  za mafunzo ya ujasiriamali na biashara ili kujijengea uwezo  wa kujiamini pale wanapoamua kujihusisha na biashara.

Ametoa wito huo akiwa kwenye mafunzo  aliyoyaandaa kwa ajili ya wakazi wa jimbo la Babati mjini  kuhusu ujasiriamali na biashara yaliyoanza leo jumatano februari 27  katika ukumbi wa Ccm babati mjini.

Amesema kwa kuwa mjini hakuna shughuli za kilimo hivyo semina hiyo itafungua njia kwa wale wanaotarajia kuanzisha biashara zao na kufanya shuguli za ujasiriamali.

Amesema semina hiyo ambayo inafanyika kwa siku tatu bila malipo katika ukumbi wa mikutano wa Ccm mjini Babati, itawasaidia wanawake na vijana kujiajiri wenyewe.

Amesema mafunzo ya ujasiriamali na biashara ni nguzo muhimu kwa vijana na Wanawake hasa wanapokuwa na malengo ya kujiajiri kwani mafunzo hutoa mwongozo.

Mbunge huyo amesema semina hiyo ameileta kwa kuonyesha  upendo alionao kwa wananchi wake huku akiwaleta wataalamu kutoka sehemu mbalimbali ambao wanatoa elimu ya ujasiriamali kwa nadharia na vitendo.

Aidha amewataka wananchi wote wa Babati wajitokeze kwa wingi kupata mafunzo hayo ambayo yanatolewa bila malipo kuanzia leo februari 27,2020 hadi februari 29.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Manyara Simon Lulu amempongeza Mbunge Gekul kwa jitihada za kuwakutanisha vijana na wanawake pamoja na kutoa mafuzo hayo ya ujasiriamali na biashara.