https://monetag.com/?ref_id=TTIb Mali: Wanajeshi 29 wafariki katika shambulizi | Muungwana BLOG

Mali: Wanajeshi 29 wafariki katika shambulizi

Wanajeshi 29 waripotiwa kufariki katika shambulizi la kigaidi Kaskazini mwa nchini Mali.

Shambulizi hilo limelenga  eneo ambalo  kunapatikana   kambi ya jeshi.

Taarifa iliotolewa na  makao makuu ya jeshi la Mali imefahamisha kuwa  shambulizi hilo limelenga pia mji wa Tarkint  Gao.

Katika shambulizi hilo la kigaidi wanajeshi 29 wamefariki na wengine watano  wamejeruhiwa.

Nchini Mali  tangu mwaka  2012 wanamgambo wa makundi ya kigaidi  wanashambulia  maeneo tofauti.