Mpinzani wa Rais Maduro arejea Venezuela

Juan Guaido, msemaji wa bunge aliejitangaza kuwa rais wa mpito nchini Venezuela arejea nchini

Mpinzani na  msemaji wa bunge la Venezuela aliejiyangaza kuwa rais wa mpito nchini  amerejea nyumbani baada ya  kukaa nje ya nchi kwa  muda wa siku 11.

 Juan Guaido aliondoka nchini Venezuela  siku moja kabla ya jaribio la kuingiza kile ambacho kilijwa kuwa msaada kutoka Marekani kupitia nchini Colombia.

Marekani ilitangaza kuwa msaada huo ni kwa ajili ya raia wa Venezuela waliokumbwa na madhila  katika maisha.

Baada ya ziara yake  nchini Colombia  Juan Guaido  alitembelea nchini Brazil, Argentina, Paraguay na Ekwado ambapo viongozi wa mataifa hayo walimuunga mkono.

Muendesha mashtaka wa Venezuela Tarek William Saab  aliomba mahakama imuwekee marufuku Juan Guaido  kuasafiri na kutaisha mali yazke .

Uturuki, Mexico, Urusi, Iran, Cuba, China na Bolivia  ndio mataifa mabyo yanamuunga mkono rais Nicolas Maduro kwa kufahmisha kuwa Maduro ndie aliechaguliwa chini  ya msingi ya demokrasia.
Mpya zaidi Nzee zaidi