Muda wowote mchezaji wa Simba SC, Ndemla kutimkia Ulaya


Kiungo wa klabu ya Simba SC, Said Ndemla, inaelezwa anatarajia kuondoka nchini kuelekea barani Ulaya kutafauta maisha mazuri zaidi ya kisoka.

Kiungo huyo mshambuliaji inataarifiwa kuwa  ataondoka kuelekea nchini Swedenkufanya majaribio na AFC Eskilstuna.
Uwanja wa AFC Eskilstun
Utakumbuka kuwa Ndemla alishawahi kufanya majaribio katika klabu hiyo na kufuzu ila hakuweza kujiunga nayo na sasa Eskilstuna wanataka kumfanyia majaribio mengine.